TAARIFA YA USHIRIKI WA NANE NANE



                                                                         
       Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania
MVIWATA – KAGERA
S.L.P 80
MULEBA- KAGERA- TANZANIA
Simu: +255 788 685 818/ +255 752 751 074

TAARIFA YA USHIRIKI WA NANENANE 2016
Banda la MVIWATA Kagera  katika maonyesho ya nanenane 2016 la kuonyesha kauli mbiu ya MVIWATA
1.Utangulizi
MVIWATA Kagera imeshiriki maonyesho ya nanenane mkoani kagera mwaka 2016 kwa kuwezeshwa na MVIWATA Taifa.
Katika maonyesho walishirikishwa wakulima watano walioweza kuonyesha :-
Ø  Ijue MVIWATA
Ø  Ufugaji wa nyuki
Ø  Ufugaji wa samaki
Ø  Ufugaji wa kwale
Ø  Shughuri zilizofanyika katika mradi wa PETS.
Jumla ya viongozi na wananchi wapatao 160 walifika katika banda la MVIWATA  Kagera kuhoji  na kupata ufahamu wa shughuri za MVIWATA kwa ujumla.

2.Shughuri Kuu Za Mviwata
Kupitia ushiriki huu,Tuliandaa vitini ,vitabu na vipeperushi  na picha vinavyoelezea shughuli kuu za  MVIWATA  na kuwapatia washiriki ili pamoja na maelezo viwasaidia kujisomea kwa uelewa zaidi:-

·         Kitini kinachoelezea shughuli za MVIWATA(fungua hapa chini)



·         Vitabu mbalimbali
Mkuu wa mkoa  Kagera Ndg Luteni general Samwel Kijuu na viongozi wa seikali wakipata maelezo ya shughuli kuu zinazofanywa na MVIWATA toka kwa promota Jovita Juston wa kikundi cha Tunaweza akiba na Mikopo Gwanseli



Vitini na vitabu mbalimbali katika kuelezea shughuli za MVIWATA


3.Ufugaji Wa Nyuki:-
Kwakuwa vikundi vinajiusisha na ujasiliamali kikundi cha chapakazi kimeonyesha kwa vitendo ufugaji wa nyuki kwa kuweka mizinga ya kisasa, mavazi ya kuzuia  usalama, Asali na vifaa vya kuvunia kama inavyoonekana hapa kweye picha-
Mkuu wa mkoa  Kagera Ndg Luteni general Samweli Kijuu na viongozi wa serikali wakipata maelezo ya ufugaji wa nyuki toka mkulima Peles Baguma wa kikundi cha chapakazi Mubunda

Mkuu wa mkoa  Kagera Ndg Luteni general Samweli Kijuu na viongozi wa serikali wakipata maelezo ya kazi za vikundi yva wakulima
4.Ufugaji wa samaki:-
Kwakuwa vikundi vinajiusisha na ujasiliamali kikundi cha Busara  kimeonyesha kwa vitendo ufugaji wa samaki  kwa kuweka vifaranga wa samaki, vifaa vya kuvunia  na chakula kama inavyoonekana hapa kwenye picha-
 Mkuu wa mkoa  Kagera Ndg Luteni general Samweli Kijuu na viongozi wa serikali wakipata maelezo yza ufugaji wa samaki toka mkulima Kajubu wa kikundi cha Busara gwanseli


5.Ufugaji wa Kwale
Kwa kuwa vikundi vinajiusisha na ujasiliamali kikundi cha Kaweso  kimeonyesha kwa vitendo ufugaji wa kwale  kwa kuweka vifaranga na mashine ya kutotoa na kwale waliofugwa  kama inavyoonekana hapa kwenye picha-

Mkuu wa mkoa  Kagera Ndg Luteni general Samweli Kijuu na viongozi wa serikali wakipata maelezo ya ufugaji wa kwale toka mkulima Kajubu wa kikundi cha Busara gwanseli

Picha ya namna ya utotoaji vifaranga vya kwale kwa kutumia incubator

6.Shughuri zilizofanyika katika mradi wa PETS.
Kupitia ushiriki huu,Tuliandaa vitini ,vitabu na vipeperushi  na picha vinavyoelezea shughuli za PETS  na kuwapatia washiriki  ili pamoja na maelezo viwasaidia kujisomea kwa uelewa zaidi:-
Ø  Kitini  kinachoelezea shughuli za PETS(fungua hapa)
Ø  Picha za matukio ya PETS
 Mkuu wa mkoa  Kagera Ndg Luteni Samweli Kijuu na viongozi wa serikali wakipata maelezo ya shughuli za PETS kutoka kwa mtendaji wa pets Mr Projestus Ishekanyoro


Picha za miradi scheme za umwagiliaji na masoko yaliokwama tangu 2006











































Ø   Picha za majukwaa  na watunga sera katika kupokea taarifa za utekekelezaji shughuri za PETS
Picha ya miche bora ya kahawa inayozalishwa na wakulima


MVIWATA  Kagera tunatoa shukrani kubwa kwa menejimenti  ya MVIWATA  kusaidia kuwezesha kifedha ushiriki wa Nanenane Bukoba 2016, kwani imesaidia kupanua wigo wa kufahamika hasa kwa vingozi wapya baada ya uteuzi wa Mhe Raisi.
                                                          
                                                   Wako,  
Projestus Ishekanyoro
K.n.y kamati ya uongozi MVIWATA Kagera

Comments

Popular posts from this blog

DONORS VIST REPORT- SOCIAL ACCOUNTABILITY MONITORING