REPORTS OF MVIWATA



Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania

(Network of Farmers’ Groups in Tanzania)
Email: mviwata.kagera@gmail.com/projemviwata@yahoo.com: Simu 0752 751074

P. O. Box 80 Muleba - Kagera
Taarifa ya Utekelezaji Shughuli za MVIWATA Kagera kwa kipindi cha Miezi Mitatu kuanzia Januari hadi Machi 2015
1. Utangulizi
 Hii ni taarifa ya shughuli za MVIWATA Kagera za miezi mitatu, Januari hadi Machi 2015. Taarifa hii inawasilishwa kwa njia ya jedwali lililopo hapa chini. Kwa ujumla shughuli hizi zinafuata Mpango Mkakati wa MVIWATA wa 2010 – 2014 na pia Mpango Kazi wa MVIWATA Kagera Januari – Disemba 2015.




Mkakati 1:   Kuimarisha vikundi na mitandao ya wakulima kwa lengo la kuwawezesha kujipanga na kujitetea.
Shughuli  iliyopangwa
Hali ya Utekelezaji
Matokeo
1.        Kuimarisha mitandao ya msingi na vikundi ili kuweza kutoa huduma kwa wanachama.
Katika kipindi cha Jananuari-March 2015, shughuli kuu iliyofanyika ni kuhamasisha uanzishwaji vikundi, mikutano mikuu ya mitandao ya misingi na vikundi na kuimalisha mitando iliyopo.

Kikundi cha AMANI Muhutwe
Mitandao ya msingi  mitano imefikiwa na nakufikia  wanachama 106 (ME 61 KE 45) kati yao wanachama wapya ni 22 (ME 14 KE 8) kama ifuatavyo:-Buganguzi (ME 7), Gwanseli 42, KE 16 ME 26 Muhutwe 11 ME 3 KE 8, Kashasha 28 KE 11 ME 17 na Mubunda 18 KE 10 ME 8.
2.      Kuada na kutoa mafunzo kwa viongozi wa mitandao na vikundi  ngazi ya kati.
Hajafanyika

3.      Kuandaa taarifa za wanachama, ulipaji wa ada za vikundi na kubaini wanachama wapya.
Kufikia tarehe 30/3/2015 tumefikia wanachama 925 wenye kadi za MVIWATA na wanachama wanufaikaji 2323 jumla 3248, vikundi 127 na mitandao 36.
Kupata wanachama wapya – vikundi 7, wanachama 22 na vikundi 7 kulipia ada ya mwaka 2015.
(orodha ya vikundi vipya na majina ya wanachama na vikundi vilivyo lipa ada imeambatanishw
Matarajio:   Kuhakikisha kuwepo Vikundi na Mitandao Imara ya Wakulima ambayo Inawajibika katika kutekeleza majukumu yao
Mkakati 2:   Ushawishi na Utetezi: kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kushawishi na kutetea maslahi yao na kuongeza ushiriki na ushikishwaji wao katika masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa katika ngazi ya msingi, kitaifa na kimataifa.
Tarajio 1:    Kuwepo mkakati wa Ushawishi na Utetezi wa MVIWATA Kagera.
1.      Kufanya tafiti mbalimbali juu ya masuala yanayogusa masilahi ya mkulima mdogo na kutoa matokeo.
·         Kukutana na watafiti wa mazao ya kilimo ili kujua chanzo cha ugonjwa wa Mnyauko wa migomba na kuutafutia ufumbuzi – ilionekana ni ugonjwa wa bacteria isiyotibika inayoenea kwa njia ya hewa.

·         Kufanyika kwa utafiti wa kushuka kwa zao la kahawa uliofanywa na watafiti kutoka SUA Morogoro Dr. Fatihiya Masawe na Ndg, Rogers Andrew kwa kushirikiana na  MVIWATA Taifa.


Sheria ya ukandishaji wa mashamba imetumika kwa kila mkulima kukata mgomba ulioathirika na kwa sasa ungonjwa wa myauko unaendelea kupungua.






Tarajio 2:    MVIWATA inatambulika vizuri kama taasisi yenye uwezo na nguvu kufanya ushawishi na utetezi kwa masilahi ya wakulima wadogo.
1.      Kuandaa na kuwezesha mafunzo ya kujenga uelewa wa wakulima juu masuala yanayoathiri ustawi wa wakulima wadogo.
Kamati ya PETS ya wilaya na Madiwani wa kata tano kushiriki mdahalo wa wa kitaifa juu ya Azimio la Umoja wa Afrika kuhusu kuwekezaji wa kilimo na usalama wa chakula lililoyofanyika Dar es salaam tarehe 28/2/2015 kwa ushirikiano wa ESAFF

Anayechangia ni Mhe. Diwani Kata Mubunda Ndg. Kalinjuma. A. Kamili
Kamati ya pets 15 Me8 Ke7 na madiwani 5 (ME) kutoka Wilaya Muleba, kujua azimio la Maputo/Malabo juu ya utekelezaji wa bajeti ya kilimo kufikia 10%.

Ndg. Projestus Ishekanyoro akiwasilisha mada ya fursa na vikwazo katika utekelezaji wa PETS Muleba
2.      Kuwezesha mafunzo ya kujengea uwezo viongozi wa vikundi na mitandao juu ya dhana ya ushawishi na utetezi ili kujenga hadhi ya taasisi ya MVIWATA Kagera.
Haijafanyika



Tarajio 3:    Kuimarisha mawasiliano na upashanaji habari ndani na nje ya MVIWATA  Kagera.
1.      Kusambaza majalida na machapisho mbalimbali ya MVIWATA hasa gazeti la pambazuko, taarifa za kila mwezi yanayohusu shughuli za shirika.
Mauzo ya jarida la pambazuko toleo no.042 hamsini yameuzwa.

Mauzo majarida Tshs 50,000/= imepokelewa

Taarifa ya utekelezaji wa shughuli za MVIWATA Kagera 2014 imetolewa.
Tarifa imepokelewa na MVIWATA Taifa, Halmashauri za Wilaya Muleba na Misenyi, Mkuu wa Wilaya Muleba na Afisa Tawala wa Mkoa.

Mkakati 3:   Kuimarisha uwezo wa kiuchumi kwa lengo la kuwezesha wakulima wadogo  kuwa na uwezo wa kiuchumi kupitia njia za akiba na mikopo, kuwaunganisha na masoko kwa kuwapatioa elimu ya ujasiriamali ili kupunguza umasikini.
Tarajio:1     Kuboresha mifumo ya masoko kwa ajili ya wakulima wadogo.
Shughuli iliyopangwa
Shughuli zilizotekelezwa
 Matokeo
Kufanyika ushawishi juu ya masoko ya zao la Ndizi  na Kahawa.
Kupitia  vikao vya watoa maamuzi kuelezea tatizo ukosefu wa masoko ya wazalishajiwadogo.
Kikao cha baraza la Madiwani Muleba
Ujenzi wa soko la Ndizi  Muleba mjini unaendelea.







Serikali imeunda timu ya utafiti wa soko la kahawa na kutoa vibali kwa wanunuzi binafsi.
Tarajio 2:    Uwezo wa wakulima umeongezeka katika huduma za kuweka nakukopa kupitia vyombo vyakuweka na kukopa.

Kuwezesha mafunzo juu ya faida za kuweka na kukopa na mbinu za uanzishwaji na uimalishaji vyombo vya kuweka na kukopa.
Mafunzo ya waweka hazina wa SACCOS yaliyoandaliwa Halmashauri ya wilaya Muleba tarehe 10 – 14/02/2015, Waweka Hazina wa SACCOS za wanachama MVIWATA tano walishiriki kwa siku nne.
Mafunzo ya Dhana ya VICOBA yaliyofanyika Mwanza tarehe 23-27/03/2015, viongozi wa SACCOS za MVIWATA Watatu wameshiriki.

Bi. Jovitha kushoto na washiriki wengine katika mafunzo ya Waweka Hazina wa SACCOS


Muleba  Farmers Network SACCOS imepata cheti safi cha ukaguzi.

Mkakati 4:   Masuala mtambuka kwa kujenga uelewa wa wakulima wadogo juu ya athari za UKIMWI, jinsia na mabadiliko ya tabia Nchi, na mwisho ujenzi wa kitaasisi kwa lengo la kuimarisha shirika la MVIWATA Kagera.
Tarajio 1:    Masuala ya VVU/UKIMWI yameingizwa katika mipango ya MVIWATA  na kuna uelewa wa kutosha kwa kwa wanachama, viongozi na watumishi.
  1. Kutoa mafunzo na uhamasishaji        juu wa wakulima kujikinga na VVU na kuwauganisha wakulima taasisi wa zinazotoa huduma ya upimaji.
Haikufanyika


Tarajio2:     Masuala kuhifadhi misitu ili kupambana na mabadiliko ya Tabia Nchi.
1.Kubaini na kutenga  hifadhi ya mistu jamii katika maeneo ya serikali za vijiji.
Kusajili mstu jamii Nyakabango na kuunda kamati ya hifadhi mistu na kupisha sheria ndogo ndogo za vijiji.
Usajili  na sheria ya kuhifadhi  umepatikana  kutoka kwa Halmashauri ya wilaya Muleba.
Mkakati 5:ujenzi wa shirika Kitaasisi:
1. Kufanya vikao vya kikatiba kwa kamati ya uongozi,kamati za PETS na kikao cha mapromota.
Kikao kimoja cha kamati ya Uongozi kimefanyika tarehe 7/1/2015.






Ø  Kupitisha mpango kazi na bajeti wa mwaka 2015
Ø  Kuandaa mpango kazi na bajeti  wa miezi mitatu
Ø  Kukagua na kuona mapato na matumizi ya mwaka 2014

Kikao cha kamati ya PETS kimefanyika
Ø  Kukusanya taarifa za PETS kutoka kata tano.
Ø  Kuandaa watakao shiriki kongamano la PETS Dar es saalam.
Ø  Kuandaa mpango kazi na bajeti wa PETS  Jan –March 2015
 2.Usimamizi na uendeshaji wa ofisi
·         Kupokea ada za vikundi  Tshs 240,000/=
·         Kupokea viingilio vya wanachama wapyaTshs 40,000/=
·         Ulipaji wa gharama za uendeshaji wa ofisi
·         Malipo ya 30% za ada  Tshs 24,000/=
·         Computer ANTIVIRUS DESK TOP and LAPTOP Tshs 40,000/=
·         Ulipaji wa pango la ofisi Jan- march 2015 Tshs 180,000/=
·         Ununuzi wa kadi za wanachama  Tshs 20,000/=



Comments

Popular posts from this blog

DONORS VIST REPORT- SOCIAL ACCOUNTABILITY MONITORING