REPORT FOR SIXTH ANNUAL MEETING -IN SWAHILI



MKUTANO MKUU NGAZI YA KATI KAGERA
UKUMBI WA CALFONIA MULEBA MJINI TAREHE 26/06/2014

MADA: PETS, UMILIKI WA ARDHI, 10% YA BAJETI YA KILIMO NA MASOKO


Baadhi ya Washiriki kushoto waliokaa Ndg. P Ishekanyoro(Mjumbe Bodi ya Taifa), J. Rwakyendera (M/Mwenyekiti , P. Ngaiza Mwenyekiti, Mhe.Lembris Kipuyo Mkuu wa Wilaya Muleba, Mr. T. Mbowe na Mr. T. Mtandu Vi Agroforestry
TAARIFA YA MAENDELEO NGAZI YA KATI KAGERA
Taarifa ilizingatia idadi ya vikundi 234 vyenye wanachama 3123, utume wa shirika, dira ya shirika, shughuli kuu zilizofanyika, mafanikio, changamoto, Mpango Mkakati wa MVIWATA Kagera, Mapato na matumizi Januari hadi Mei 2014 na ombi kwa mgeni rasmi iliyowasilishwa na Mwenyekiti MVIWATA Kagera Ndg. Ponsian Ngaiza. Mkutano huu walishiriki wanachama 50 ME 33, KE 17, Wataalamu wa kilimo na misitu pamoja na wageni toka Vi Agroforestry
UFUNGUZI WA MKUTANO MKUU
Mgeni rasmi Mhe. Mkuu wa Wilaya Ndg. Lembris Kipuyo, kabla ya ufunguzi wa mkutano, alishukuru uogonzi na wanachama wa MVIWATA Kagera kumualika katika mkutano huu muhimu.
Katika hotuba alipongeza jitihada zinazofanywa na MVIWATA TAIFA kuwaunganisha wakulima kuwa na sauti moja,pia Mgeni rasmi kuwaekeza wakulima kuwa na  mipango mikubwa endelevu ikiwemo miundo mbinu,masoko na viwanda.
Mgeni rasmi alitoa agizo kwa wataalamu waliomo wilayani  kushirikiana na wakulima kutatua changamoto zinazowakabili wakulima katika shughuli za uzalishaji ikiwemo suala la PETS, Masoko, Magonjwa ya mimea kama Myauko, umiliki wa aridhi na hifadhi misitu jamii na kuhaidi ushirikiano mkubwa pale atakapohitajika pamija na kuweka mawasiliano yake wazi. Baada ya hapo mkutano umefunguliwa saa 4:30 asubuhi.



MADA KUU ZA MKUTANO

1.   Wakulima juu ya Mapato na Matumizi ya Pesa za Umma (PETS)
Trainer of Trainers (TOT) Ndg. Projestus Ishekanyoro aliwashirikisha washiriki wa mkutano maana ya PETS, faida za PETS, haki za mkulima kushiriki PETS na changamoto wanazokumbana nazo katika utekelezaji wa PETS.

Ndg. Projestus Ishekanyoro akiwasilisha Mada ya PETS katika Mkutano Mkuu MVIWATA Kagera

2.   Ushiriki wa Mkulima katika Bajeti ya Serikali
Mada hii iliwasilishwa na Ndg. D.W. Lwekamwa (PAFOI)  ambapo aliwashirikisha wajumbe wa Mkutano Mkuu kwa kuwafafanulia kuwa zamani Mipango ilikuwa ikipangwa kuanzia ngazi za juu (TOP BOTTOM APPROACH ambayo miradi mbalimbali haikuwa endelevu kwa kuwa haikuwa hitaji la wakulima. Kwa sasa bajeti ni shirikishi (BOTTOM UP APPROACH).


3.  Wajibu wa Kuhifadhi Misitu Jamii

Mada husika iliwasilishwa na Ndg. Lugano Ambakisye (FO) ambapo alitoa changamoto za kimazingira zinazowakabili wakulima kutokana na mabadiliko ya tabia nchi hali inayochangiwa na uhifadhi duni wa misitu. Aliwasihi wakulima watenge maeneo ya uhifadhi wa misitu jamii na kuzifuata sheria zilizopo ili kwa pamoja kupambana na mabadiliko ya tabia nchi kwa uzalishaji endelevu.


4.  Madhara ya na jinsi ya kupambana na Ugonjwa wa Myauko wa Migomba
Ndg. Daudi Kingu (Afisa Kilimo) alielezea madhara ya Mnyauko wa Migomba, hatua zilizochukuliwa mpaka sasa na kuwaomba wakulima kuchukua hatua za awali ambazo ni kuondoa maua dume, kukata na kuchimbia mgomba ulioathirika na tayari sheria ipo kwa watakaopuuzia kuchukua hatua.



Comments

Popular posts from this blog

DONORS VIST REPORT- SOCIAL ACCOUNTABILITY MONITORING